Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akiwa kwenye ziara katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST) kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya mradi wa ukarabati wa uwanja wa michezo wa LST unaotarajiwa kutumika kwa mazoezi kwenye mashindano ya mchezo wa mpira wa miguu ya CHAN 2025 na AFCON 2027. Ziara hiyo imefanyika tarehe 05 Juni, 2025.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Eliakim Maswi (katikati) akiimba wimbo wa wafanyakazi pamoja na viongozi wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST) wakati wa ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi wa LST lililofanyika tarehe 3 na 4 Aprili, 2025 jijini Dodoma.
Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST) tarehe 22 Novemba, 2024 imepokea ujumbe (delegation) kutoka Mahakama Kuu ya Watu ya Jimbo la Zhejiang ya nchini China. Lengo la ujumbe huo lilikuwa ni kujadili namna ya kuanzisha mashirikiano na kubadilishana uzoefu. Ujumbe huo ambao uliongozwa na Makamu wa Rais Mtendaji wa Mahakama hiyo pia ulipata nafasi ya kutembelea maeneo mbalimbali ya Taasisi pamoja na kukutana na Menejimenti.
Balozi wa Shirikisho la Urusi nchini Tanzania, Andrey Avetisyan akizungumza katika mhadhara wa kitaaluma kutoka kwa Wataalamu wa Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Urusi tarehe 30 Aprili, 2024 katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo (The Law School of Tanzania).
Aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria wa kipindi hicho, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiwa kwenye picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya LST, Menejimenti na Wahitimu wa Kozi ya Astashahada ya Wasaidizi wa Kisheria katika mahafali yao yaliyofanyika katika viwanja vya Taasisi tarehe 27 Machi, 2024.
Wanafunzi wa Law School wakiwa kwenye mafunzo kwa vitendo
Baadhi ya wahitimu wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST) wakila kiapo cha Uwakili mbele ya Jaji Mkuu wa Tanzania.