Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Katiba na Sheria

Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST)

lst Logo
Majukumu ya Taasisi

Majukumu ya msingi ya Taasisi yameainishwa katika kifungu cha 5 cha Sheria ya Taasisi Sura ya 425 ambayo ni:

  • Kutoa, kuendesha na kusimamia mafunzo ya unasheria kwa vitendo chini ya usimamizi wa Baraza la Elimu ya Sheria nchini (the Council of Legal Education).

  • Kuweka mazingira na miundombinu itakayowezesha utoaji elimu ya uanasheria kwa vitendo

  • Kuendesha mitihani na kuwatunukia vyeti wahitimu wa mafunzo ya uanasheria kwa vitendo.

  • Kudhamini, kupanga, kutoa vifaa kwa ajili ya kuendesha semina, makongamano na mikutano katika masuala yanayohusu sheria

  • Kutoa machapisho mbalimbali ya shughuli zinazohusiana na Bodi ya Uendeshaji ya Taasisi

  • Kufanya tafiti za kisheria kwenye maeneo mahsusi kama itakavyoamuliwa na Bodi ya uendeshaji ya Taasisi.

  • Kutumia matokea ya tafiti hizo kuboresha mafunzo ya uanasheria kwa vitendo, fasihi na uboreshaji wa mtaala na ufundishaji.

  • Kutoa ushauri elekezi kuhusu masuala ya kisheria kwa Serikali, umma na taasisi binafsi, na kwa mtu mmoja mmoja ndani na nje ya nchi

  • Kutangaza machapisho mbali mbali ambayo yanatokana na kazi mbalimbali zinazofanywa na Taasisi kama itakavyoamuliwa na Bodi ya uendeshaji ya Taasisi

  • Kudhamini na kutoa vifaa kwa ajili ya mafunzo ya muda mfupi kulingana na mahitaji ya ndani na umma.

  • Kuanzisha ushirikiano na vyuo na taasisi zingine zote za kitaifa na kimataifa

  • Kufanya shughuli nyingine za kisheria kama itakavyoekelezwa na Bodi ya Uendeshaji wa Taasisi.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
https://saris.lst.ac.tz/Registrations

" >